Gazeti na serikali nchini Zimbabwe la - The Herald - halijaandika chochote kuonyesha yakle ambayo yamekuwa yakiendelea usiku kucha.
Bado mtandao huo una taarifa zinazoonekana kumuunga mkono Rais Robert Mugabe.
Taarifa yake kuu inamnukuu kiongozi wa wa vijama katika chama cha Zanu-PF Kudzai Chipanga akimunga mkon Rais Mugabe, alisema tunampigania Rais kwa masha yetu."
The Herald
Magari ya kijeshi yanaonekana yakipiga doria katika barabara za mji mkuu wa Zimbabwe Harare.
Picha zilizochukuliwa mapema leo zinaonyesha magari ya kijeshi na wanajeshi, wakionekana kuelekeza au kuzuia magari.
Reuters
Reuters
Akaunti ya chama cha Zanu PF inasemama kuwa Emmerson Mnangagwa amefanywa kuwa rais wa mpito.
Mnangawa mwenye umri wa miaka 75 alifutwa kama makamuu wa rais kutokana na kile serikali ilisema kuwa kutokuwa mtiifu.
Kufutwa kwake kulionekana kama nia ya kumwezesha mke wa Rais Mugabe, Grace, kufuata nyayo za mumewe na kuwa kiongozi wa Zimbabwe.
Awali alikuwa ametoa wito kwa mumewe kumfuta makamu wa rais.
Bw. Mnangagwa ambaye ni mku wa zamani wa ujasusi amekuwa mtu ambaye alitarajiwa kumrithi Rais Mugabe 93.
Kufutwa kwake kulimaanisha kuwa Grace Mugabe anatarajiwa kuteuliwa kuwa makamu wa rais wakati wa mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi ujao.
AFP
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani saa chache baada ya jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka, kwa mujibu wa mtandao maarufu wa habari nchini Afrika Kusini.
"Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani," mtandao wa wa News24 uliandika bila ya kutoa taarifa zaidi.
Misukusuko ya kisiasa imekuwa ikiongezeka tangu Mugabe hivi majuzi amfute Emmerson Mnangagwa, mshirika wake wa miaka mingi kama makamu wa Rais.
Jeshi la Zimbabwe lilisoma taarifa kwenye kituo cha runinga cha serikali ZBC, likisema kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu.
Hata hivyo limesema kuwa hayo sio mapinduzi ya kijeshi na Rais Mugabe yuko salama.
Milio mikubwa ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu Harare mapema leo.
Taarifa hiyo ya jeshi ilikuja saa kadhaa baada ya jeshi kudhibiti kituo cha ZBC.
Mwanamume mmoja ambaye alikuwa amevaa sare za jeshi alisema kuwa jeshi linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.
"Wakati tutakapomalzia wajibu wetu, tunatarajia kuwa hali itadudi kuwa sawa."
Taarifa hiyo ilisema kuwa Mugabe 93, na familia yake wako salama.
Haijulikani ni nani anaongoza hatua hiyo ya kijeshi.
Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yanaonekana maeneo ya mjini Harare.
Hali hiyo ya wasi wasi wa lolote kuweza kutokea, imeanza hapo jana jioni, ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa pamoja na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe ZBC.
'Mapinduzi ya kijeshi' Zimbabwe
Reviewed by EXUPER ASSOCIATION
on
November 15, 2017
Rating:
No comments: