To Advertise here call +255786419829

To Advertise here call +255786419829

Wakazi wa jiji la Dsm wametakiwa kujitokeza kuanzia Nov.20 katika Upimaji Afya kwenye meli kubwa ya Jeshi la majini la China

Image result for MAKONDA NA WANAJESHI WA CHINAWakazi wa jiji la Dsm wametakiwa kujitokeza kuanzia Nov.20 mwaka huu katika Upimaji Afya ,kupatiwa matibabu ya Upasuaji mdogo na Mkubwa Bure utakaofanyika katika meli kubwa ya Jeshi la majini la China ambayo itakuwa na madaktari bingwa pamoja na wahudumu zaidi ya 385.
Mkuu wa Mkoa wa Dsm Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari pamoja na makamanda wa jeshi la Majini la China ambao tayari wamewasili amesema,kuwasili kwa meli hiyo kutokana na balozi wa China aliyemaliza Muda wake Dr.LU ambae alijionea mafuriko ya wananchi katika Upimaji afya katika Viwanja vya Mnazi mmoja miezi mitatu iliyopita na Kuahidi kuleta madaktari kuunga Mkono jitihada za Bw,Makonda.
Aidha makonda amewataka wananchi waliokuwa wakisubiri kufanyiwa Upasuaji katika hospitali za m/myamala,temeke na amana ambao wako katika foleni ya kusubiri kufika katika meli hiyo ili kufanyiwa upasuaji huku ikiwa na Vifaa vya kisasa vya Tiba.
Meja Chi Song Kutoka katika kikosi cha jeshi la majini katika meli hiyo ambayo ni kubwa kuliko meli zote zilizowahi kuingia hapa nchini amesema Matibabu hayo ya bure ni matokeo mazuri ya Ushirikiano katika ya Tanzania na China pamoja na waasisi wa nchini hizo.
Wakazi wa jiji la Dsm wametakiwa kujitokeza kuanzia Nov.20 katika Upimaji Afya kwenye meli kubwa ya Jeshi la majini la China Wakazi wa jiji la Dsm wametakiwa kujitokeza kuanzia Nov.20 katika Upimaji Afya kwenye meli kubwa ya Jeshi la majini la China Reviewed by EXUPER ASSOCIATION on November 14, 2017 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.